Monday 01 October 2021

00:00:00

Pentecostal Assemblies of God (Tanzania)

image of Askofu

Kanisa la Kipentekoste lenye msingi na imani katika Neno la Mungu linaloundwa na ujumla wa makanisa mahalia pamoja. Lilianzishwa chini ya wamisionari kutoka Kanada wakiwa chini ya Shirika la kimisionari liitwalo Pentecostal Assemblies of Canada ambao walianza kueneza Injili Tanganyika katika miaka ya 1912 ambapo katika miaka hiyo wengine walifariki kwa magonjwa.

Mnamo mwaka 1950, wahubiri wa mwanzo wa Tanganyika walipewa mafunzo. Kanisa lilianza katika mkoa wa Mara na kuanzisha shule ya Biblia pale Nyasirori Butiama. Wakati huo lengo kuu lilikuwa kuhubiri Injili na kuanzisha makanisa. Kanisa liandikishwe rasmi mnamo tarehe 14 Aprili mwaka 1967 na kupata "Cheti cha Ithibati"

Kanuni Yetu ya Imani

  1. Kwamba kuna Mungu mmoja mwenye enzi ya milele katika Utatu: Mungu Baba,Mungu Mwana,na Mungu Roho Mtakatifu. (Kumb 6:4; Mk 12:29; Mt 28:19; 2Kor 13:14).
  2. Katika uumbaji mkamilifu wa Mungu kwa binadamu, mume na mke, kwa mfano wake, na viumbe vyote, na kwamba kulikuwa na anguko la malaika na mwanadamu ambalo matokeo yake yameleta maumivu na uharibifu na kifo cha kiroho na cha kimwili. (Mwa 1:1, 26-27, 31; 3:1-19; Rum 3:23).
  3. Biblia imevuviwa na Mungu,ni Neno la Mungu lenye mamlaka na lisilokuwa na makosa nayo ndiyo msingi wa imani yetu na mwenendo wa kikristo. (2Tim 3:15-17; 2Pet 1:21).
  4. Katika Uungu wa Bwana wetu Yesu Kristo,katika kuzaliwa kwake na bikira huyo ni Mariamu,katika maisha yake yasiyo na dhambi,katika miujiza yake,katika kifo chake badala ya wenye dhambi ambacho kilifanyika upatanisho kati ya mwanadamu na Mungu, na katika ufufuo wake katika mwili na kupaa kwake mbinguni na kukaa mkono wa kuume wa Mungu Baba,na katika kurudi kwake mara ya pili hapa duniani katika nguvu na utukufu ili kuyatawala Mataifa. (Mt 1:18-23; 16:15-16; Mk 16:19; Mdo 1:9-11; 2Kor 5:17; Kol. 1:15).
  5. Kwamba njia pekee ya wokovu wa binadamu kutoka dhambini ni kutubu na kuacha dhambi na kumwamini Bwana Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake na kwa kuzaliwa mara ya pili kwa Roho Mtakatifu. (Yoh 1:11-13; 3:5-8; Mdo 2:38; Rum 10:9; 1Yoh 1:9).
  6. Katika kuponywa kwa mwili wa binadamu ambako kumepatikana kwa njia ya kifo cha Yesu Kristo pale msalabani,na uponyaji huo hupokelewa kwa ombi la imani. (Isa 53:1-5; Mk 16:16-18).
  7. Katika ubatizo wa Roho Mtakatifu pamoja na ushuhuda wa kunena kwa lugha kunakofua -tana na Tunda la Roho, kunakopokelewa kwa imani ikiambatana na masharti ya Biblia ya kupokea ubatizo huo. (Yoh 7:37; 14:16-17; 16:12-15; Mdo 1:8; 2:1-4; 10:44-47; 19:2-6).
  8. Kanisa ni watu walioitwa na Mungu kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kutoka ulimwenguni na kuwekwa wakfu kwa ajili yake, kwa kuzaliwa mara ya pili na kuunganishwa katika mwili wa Kristo, ambaye ni kichwa cha Kanisa. Kazi ya Kanisa ni kumpenda na kumtukuza Mungu na kuhubiri Injili kwa kila kiumbe na kuishi katika tumaini la ufufuo wa wafu. (Mt 5:13-14; Yoh 15:1,2; Mdo 1:8; Efe 1:7,22; 4:11-16; 5:23; 2Kor 6:6-18).

Historia ya Kanisa PAG (Tanzania)

Historia kamili inaonesha kuwa wamishenari wa kwanza kabisa kutoka Kanada waliingia Tanganyika miaka ya 1913, na kuanzisha kazi ya Mungu maeneo ya Itigi, mkoani Singida, lakini kazi hiyo haikusimama. Katika mwaka 1940 baadhi ya wakristo kutoka Kenya ndugu Elly Osumba na wenzake wanne wakahamia Tanganyika mkoa wa Mara huko Bugwema, Nyangombe Majita, wakaanza ibada ya jumapili chini ya mti. Mwaka 1944 Mwinjilisti kutoka Kenya Athanasio Odenyo Okech akaja kusaidia kazi hiyo. Jengo la kanisa la kwanza la miti lilijengwa mwaka 1946 na wakati huohuo kanisa la Pentecostal Assemblies of God Kenya wamisionari wawili Rev. Morrison na Rev. J. Liny na wachungaji wawili Rev. Charles Muga na Rev. James Gorgor wakafanya ubatizo wa kwanza Tanganyika. Walibatiza watu kumi, kanisa wakati huo linaitwa Pentecostal Assemblies of God East Afrika (PAGEA).

Juhudi na taabu walizopata watumishi wenzetu waliopita wakimtegemea Mungu, matunda yake ndiyo haya yanayoonekana hivi leo. PAG (Tanzania) tulijitegemea wenyewe mwaka 1967 na kupata cheti cha ithibati “Certificate of Incorparation” tarehe 14/04/1967. Uchaguzi mkuu wa kwanza ulifanyika oktoba 1967 na akachaguliwa Askofu mkuu wa kwanza Rev. Jacson Magarinza. Uchaguzi mkuu wa pili mwaka 1969 – Askofu mkuu Rev.Herman Ndenda. Uchaguzi mkuu wa tatu na nne 1971-1975 – Askofu mkuu Rev. Jacson Magarinza. Uchaguzi wa mkuu wa tano na sita 1975-1978 – Askofu mkuu Rev. Stephen Omoso. Uchaguzi mkuu wa saba, nane, tisa, na kumi 1979-1985 – Askofu mkuu Rev. Daniel Itaja. Uchaguzi mkuu wa kumi na moja, kumi na mbili na kumi na tatu mwaka 1993-2005 Askofu Rev. Francis Rwechungura. Uchaguzi wa kumi na nne mwaka 2005-2010 Kanisa likiwa pande mbili upande moja alichaguliwa Askofu Rev. Daniel Awet. Na upande mwengine akachaguliwa Askofu Thomas Faida. Mwaka wa 2013 ukafanyika uchaguzi wa kumi na tano wa pamoja akachaguliwa Askofu Dr. Daniel Awet.

VIONGOZI WAKUU

Event Picture
REV. DKT. DANIEL A. ALLEY

ASKOFU MKUU PAG (T)

"Yeremia 33:3" "Niite, nami nitakuitikia na kukuonyesha mambo makubwa yaliyo fichika ambayo hujapata kuyajua"

Rev

REV. THOMAS Y. FAIDA

Makamu Askofu Mkuu
Rev

REV: SHUKRANI W. RUTONDA

Katibu Mkuu
Rev

REV: CHARLES M. KANYIKA

Naibu Katibu Mkuu
Rev

EV: PHILIP S. AMOS

Afisa Utawala

VIONGOZI WA IDARA MBALIMBALI

Dondoo Muhimu

Maeneo Makuu ya Kimkakati

Ibada na uanafunzi    
Kuendesha ibada hai na zenye mvuto ambazo zimejawa na uwepo wa Roho Mtakatifu, ubora katika kila eneo (uimbaji, ushemasi, matangazo, kutunza muda, mafundisho na mahubiri sahihi n.k. ), yanayolenga kuleta mabadiliko ifikapo 2031
Rejea Mpango Mkakati
Kuongeza kwa kasi idadi ya makanisa ya PAG (T) kutoka 1,717 hadi 11,161 na washirika kutoka 56,794 hadi 585,850 kupitia juhudi za pamoja za uinjilisti, kupanda makanisa, na umisheni kwa uweza wa Roho Mtakatifu ifikapo 2031
Rejea Mpango Mkakati
Kuimarisha ubora wa elimu ya theolojia kwa kutumia njia za kisasa na mipango mseto zitakazoleta viongozi wa kikristo wazuri zaidi na imara (wasio rasmi 0 hadi 2,790, wenye cheti 721 hadi 7,812, stashahada 83 hadi 335, shahada 41 hadi 112, shahada za uzamili 9 hadi 56 na shahada za uzamivu 2 hadi 10) ambao watakuwa mawakala wa mabadiliko katika kutimiza Agizo Kuu ifikapo 2031
Rejea Mpango Mkakati
Kuimarisha ndoa na familia kwa kutoa mafundisho sahihi ya kibiblia kupitia semina, warsha, makongamano na njia nyingine zifaazo.
Rejea Mpango Mkakati
Kuwaandaa watoto na vijana wamchao Mungu kupitia programu sahihi zilizovuviwa na nguvu za Roho Mtakatifu na shuguliza zinazowapatia fursa kuibua vipaji vyao kama mabalozi wa Kristo na wakala wa mabadiliko ifikapo 2031.
Rejea Mpango Mkakati
Kuanzisha programu za kijamii za maendeleo na miradi zinazowawezesha maskini na makundi ya waishio katika mazingira magumu kupata msaada kamili (kiroho na kimwili) kiuhalisia ifikapo 2031.
Rejea Mpango Mkakati
Kuanzisha na kuimarisha ubia (ushirika-wenza) na ushirikiano imara na mashirikina yenye mtazamo unaoendana kimaono, shabaha, tunu na malengo ili kutimiza malengo PAG (T) ifikapo 2031.
Rejea Mpango Mkakati
Kuongeza matumizi ya vyombo vya habari na teknolojia ambayo itakayoongeza ufanisi na ubora katika kutimiza dira na dhamira ya PAG (T) ifikapo 2031.
Rejea Mpango Mkakati
Kuimarisha na kuweka sera na mifumo ya fedha ambayo itawezesha upatikanaji wa rasilimali-fedha na vitu, uwazi, uwajibikaji, ili kuleta hamasa na kuwavutia washirika wa PAG (T), washirika-wenza, na wawekezaji ifikapo 2031.
Rejea Mpango Mkakati
Kuwezesha utawala uliojaa nguvu za Roho Mtakatifu na uwazi utakaoleta mabadiliko, ufanisi na uongozi wenye maono utakaoleta ukuaji, uwezesho na uwajibikaji katika ngazi zote ifikapo 2031.
Rejea Mpango Mkakati

Yaliyojiri

Event Picture
Zawadi Kwa Viongozi

Askofu Mkuu na Mhasibu Mkuu wakizawadiwa na Kanisa Soma zaidi

Ambapo walizawadiwa kila mmoja Nguo za Kiasili katika kanisa la GITING Mkoani Manyara.

Event Picture
Uinjilisti

Ev. Philip S. Amos katika majukumu ya uinjilisti katika viwanja vya makulu... Soma zaidi

Katika mkutano huo watu zaidi ya 100 walikubali kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wao na kuongozwa sala ya toba.

Event Picture
Msaada kwa wahitaji

Tukio hili limefanyika katika kanisa la Luhembe na Mruklazo (Jimbo la Kagera wilaya ya Ngara), ambapo msaada wa vifaa mbalimbali vya shule kama daftari na vinginevyo Soma zaidi

vimetolewa kwa watoto 50 wa shule za msingi na sekondari ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kanisa la PAG (T) kusaidia familia masikini

Event Picture
Misaada

Ni makabidhiano ya gari. Soma zaidi

Mgeni Rasimi Rev. James KESANTA, akimkabidhi Gari la Jimbo la Dodoma Askofu wa Jimbo la Dodoma Bishop Joel Nondi. Tukio limefanyika kwenye Ukumbi wa DCC

Picha mbalimbali

Warsha
Kusimika wachungaji
Askofu mkuu awasimika Wachungaji jimbo la Geita
Image 2
Wajumbe Manyara
Wajumbe wa Kongamano la Wachungaji Jimbo la Manyara
Waangalizi
Baraza la Waangalizi
Kikao cha halmashauri Kuu na Baraza la Waangalizi kilichofanyika Kanisa la DCC Dodoma, 1-2, machi 2023
Image 4
Hati ya Pongezi
Askofu mkuu Dr. Daniel Awet afanya Ziara ya kikazi katika nchi ya Burundi na hapo apewa Hati ya Pongezi na Askofu mkuu wa Burundi kwa kazi njema anayofanya ya Umisheni.
Image 5
Uondozi Jimbo la Geita
Picha ya pamoja Askofu mkuu, Wasimikwa na Uongozi wa Jimbo la Geita
Image 6
Uzinduzi wa gari la Idara
Mkurugenzi wa idara ya Wanawake wilaya ya Hanang Mch. Yustina Yona akiendesha gari lililo zinduliwa na Baba Askofu Mkuu.

Wasiliana nasi